Chama
cha Wananchi (CUF), upande wa Profesa Ibrahim Lipumba kimewaomba
radhi wapiga kura wa jimbo la Kinondoni baada ya aliyekuwa mbunge wa
jimbo hilo kupitia chama hicho, Maulid Mtulia kujiuzulu.
Kauli
imetolewa leo, Jumatatu Desemba 4, 2017 na Mkurugenzi wa Habari,
Uenezi na Mawasiliano ya Umma, Abdul Kambaya wakati akizungumza na
wanahabari kwenye makao makuu ya chama hicho Buguruni.
Amesema
CUF iliwaaminisha wakazi wa Kinondoni kwa kumpeleka Mtulia kugombea
jimbo hilo kwa kuwa ni mtu makini na mambo mengi alishaanza kuyatekeleza
ikiwamo kuzuia bomoa bomoa lakini wanasikitika kujiuzulu kwake.
"CUF
haikutarajia kuingia katika uchaguzi mdogo hasa jimbo la Kinondoni
kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 labda kingetokea kifo. Tunawaomba
radhi wakazi wa Kinondoni," amesema Kambaya.
Kambaya amesema sababu za kujiuzulu alizozitoa Mtulia ni za msingi kwake lakini kwao hazina maana wala mashiko.
Desemba
2, Mtulia alitangaza kujiuzulu nafasi ya ubunge huku akisema amefikia
uamuzi huo bila kushawishia na mtu yoyote na ameamua kuhamia CCM.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )