Uamuzi wa Maulid Mtulia kujivua ubunge na uanachama haujakishtua chama chake cha CUF, badala yake kimesema bado wengine wawili ambao kingependa waondoke haraka.
Hilo
lilisemwa jana na katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ambaye
anaongoza upande mmojapo kati ya mbili zinazokinzana. Upande mwingine
unaongozwa na Profesa Ibrahim Lipumba.
Naibu
katibu mkuu wa CUF (Zanzibar), Nassor Ahmed Mazrui amesema kuwa, Mtulia
ni mmoja wa wabunge watatu wanaomuunga mkono Profesa Lipumba.
“Hatukutarajia
kama Mtulia ataondoka wakati huu, bali tulijua ataendelea kudumu.
Lakini kama ameondoka ni faraja kwetu kwa sababu katika mipango yetu
tulishamuondoa,” alisema Mazrui.
“Tunawaombea
dua wale wawili waliobaki waondoke hata leo kwa sababu kuendelea kukaa
kwao ndani ya CUF ni kukidhoofisha chama hiki.”
Mazrui
aliwataka wabunge kutoshangaa endapo wenzao hao watatangaza kujiuzulu
nafasi zao akidai kuna mipango inaendelea kupangwa ili kufanikisha
mchakato huo.
“Narudia
tena na waondoke, tena waondoke haraka. Ninawahakikishia wana CUF kuwa
chama hiki kipo imara na wasiwe na hofu,” alisema Mazrui.
Alisema
CUF ni taasisi imara na kati ya wabunge 40, watatu alidai wamekuwa
wakikivuruga chama hicho kwa kushirikiana na Profesa Lipumba.
Akizungumzia kuondoka kwa Mtulia, alisema wakati mwingine akifa mgonjwa uliyemuuguza muda mrefu unamshukuru Mungu.
“Tunamshukuru Mungu maana tumeuguza vya kutosha. Haikuwa bahati yetu,” alisema.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )