Wanafunzi
wa darasa la saba wameshindwa kufanya hesabu za darasa la pili baada ya
kubainika ni asilimia 69 pekee wanaoweza kufanya hesabu hizo. Pia
asilimia 48 tu ya darasa la tatu wanaweza kufanya hesabu za darasa la
pili
Aidha,
asilimia 38 ya wanafunzi wa darasa la tatu ndiyo wanaoweza kusoma
hadithi ya kingereza ya darasa la pili na asilimia 82 ya wanafunzi wa
darasa la saba wamebainika kuweza kusoma hadithi ya Kiingereza ya
darasa la pili.
Utafiti
huo kwa mujibu wa taasisi ya Twaweza ulifanyika katika wilaya 159
ukishirikisha sampuli ya watoto 112,455 wenye miaka kati ya saba hadi
16.
Akizindua
ripoti hiyo jana Desemba 3 katika shule ya msingi mazoezi afisa tawala
wilaya ya Monduli, Sharif Mziray alisema kwamba serikali imeipokea
ripoti hiyo kwa mikono miwili na imewasaidia kuwafungua mambo mengi.
Mziray,
alisema kwamba serikali inaichukulia ripoti hiyo kama changamoto na
kuanzia sasa watatengeneza mazingira wezeshi kwa walimu na wanafunzi ili
kujenga mazingira bora ya watoto kujifunza.
“Hii
ni changamoto kwetu sisi kama serikali ya wilaya lakini wazazi pamoja
na walimu mna changamoto ya kuhakikisha mnaweka mazingira mazuri ya
watoto kujifunza”alisema Mziray
Hata
hivyo, mratibu wa programu ya Uwezo wilayani Monduli, Mohammed Nkinde
alisema kwamba wilaya hiyo imeshika nafasi ya 43 kati ya 159 katika
ngazi ya kitaifa na nafasi ya 4 katika ngazi ya mkoa katika uwezo wa
watoto kujifunza.
Nkinde,
alisema kwamba mahudhurio ya walimu na ufundishaji kwa ujumla upo chini
wilayani Monduli kwa kuwa kiwango cha mahudhurio wilayani humo
kinaonyesha kuwa ni asilimia 86 ya mahudhurio ya walimu na asilimia 75
ya mahudhurio ya wanafunzi kiwango ambacho hakiridhishi.
“Hii
inaonyesha kwamba muda wa wanafunzi na mwalimu kukutana au kufundisha
darasani wakati wa muda wa shule ni mdogo na hivyo wanafunzi hawapati
muda unaopaswa kufundishwa ili waweze kujifunza stadi za msingi”
alisema Nkinde
Ofisa
maadili na nidhamu kutoka tume ya utumishi wa walimu wilayani humo,
Rhoda Msemo alikemea tabia ya baadhi ya wazazi ambao hawakubahatika
kwenda shule kutokagua madaftari ya watoto wao na kusema tabia hiyo
haifai.
“Kuna
baadhi ya wazazi hawakupata bahati ya kwenda shule hivyo wanawaogopa
watoto wao hata kukagua home work (kazi za nyumbani) hawakagui hii si
sawa kagueni kazi zao hawa watoto msiwaogope” alisema Msemo
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )