Staa
wa soka wa kimataifa wa Ivory Coast aliyewahi kuvichezea vilabu
mbalimbali Ulaya kama Arsenal na Galatasaray ya Uturuki Emmanuel Eboue
amedai kufilisika baada ya talaka, iliyompa mali zote mkewe Auerilie Bertrand
Eboue kwa sasa ana umri wa miaka 34 na anaitumikia adhabu ya kufungiwa mwaka mmoja na FIFA kwa kushindwa kumlipa wakala wake.
Eboue
licha ya kutokea katika maisha magumu Ivory Coast alifanikiwa
kutengeneza pesa nyingi akiwa katika Ligi Kuu England akiitumikia
Arsenal kwa miaka saba.
Beki
huyo wa zamani wa Arsenal kwa sasa yupo katika maisha magumu na analala
chini kwa rafiki yake huku akishindwa kulipia pesa nguo zake ziende dry
cleaner, hivyo analazimika kufua kwa mikono. Eboue anatajwa kuelekea
kufilisika kutokana na kutalakiana na mkewe.
Hali hiyo imemfanya Eboue kuwa masikini kutokana na utajiri wake wote kumuandikisha mkewe.
Kisheria
wakiachana mali zote zitakuwa za mwanamke ambaye amezaa nae watoto
watatu, jambo ambalo Eboue linamfanya aumie kichwa na kuweka wazi kuwa
mara kadhaa linamjia wazo la kujiua kichwani kwake na anaomba Mungu
aliepuke.
Eboue ameichezea Arsenal kwa miaka saba kabla ya mwaka 2011 kuamua kujiunga na Galatasaray ya Uturuki.
“Pesa
zote ambazo nilikuwa naingiza nilikuwa natuma kwa mke wangu kwa ajili
ya watoto wetu, nikiwa Galatasaray Uturuki nilikuwa naingiza euro
milioni nane na nilikuwa namtumia euro milioni 7, chochote alichokuwa
anataka nisaini nilikuwa nasaini”-Eboue
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )