Leo
 Jumanne Novemba 6, 2018, mbunge wa Temeke (CUF), Abdallah Mtolea 
ameuliza kama Serikali haioni kukimbiza Mwenge wa Uhuru kwa sasa hakuna 
umuhimu tena kwani umekuwa ukisababisha mambo mengi ikiwemo magonjwa ya 
zinaa ikiwamo HIV.
Akiuliza
 swali katika kikao cha kwanza, mkutano wa 13 wa Bunge unaoendelea 
jijini Dodoma, Mtolea alielekeza swali hilo kwa Waziri Mkuu kuwa kama 
Mwalimu Nyerere alisema anawasha mwenge ili uwekwe juu ya mlima 
Kilimanjaro kwanini serikali inaendelea kuutembeza.
Akijibu
 swali hilo kwa niaba ya Waziri Mkuu, Naibu Waziri wa Kazi Kazi, Vijana,
 Ajira na watu wenye ulemavu Anthony Mavunde amesema "kuwa lengo la 
mwenge ni kujenga misingi ya binadamu na utu wa mtanzania, pia umelenga 
kuhamasisha ukombozi wa bara la Afrika, kupitia utaratibu huu, mwenge ni
 chombo muhimu kwa kuimarisha nchi yetu.”
Mara
 baada ya majibu hayo Mbunge huyo wa jimbo la Temeke alidai mwenge huo 
kwa sasa unapokelewa na baadhi ya watumishi wa serikali, wakiwemo 
madiwani pamoja wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari pekee akidai 
kuwa wananchi wamechoshwa kuuona kila mwaka.
Kufuatia
 swali hilo la Nyongeza Spika Ndugai aliamua kumkatisha mbunge huyo wa 
Temeke kwa kile alichokisema kuwa swali lake halikuwa la msingi.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
 

 
 
 
 
 
 
 
