Featured
Loading...

Chris Brown aingia tena matatani huko Ibiza

Chris Brown ameendelea kucheza na mdomo wa sheria kwa kufanya uharibufu wa nyumba huko Ibiza. chris-brown-ibiza
Staa huyo alikodi nyumba moja wiki iliyopita huko Villa, Ibiza alipokwenda mapumzikoni akiwa na watu wake. Mwenye nyumba hakuridhishwa na muonekano wa nyumba yake baada ya msanii huyo kumaliza muda wake wa kukaa kwenye nyumba hiyo.
Mwenye nyumba pia amedai kuwa amekuta ukuta wa nyumba yake umechafuliwa vibaya huku kukiwa kumefanyika uharibifu mkubwa ndani ya nyumba yake hiyo na hivyo ametaka kulipwa kiasi cha dola 60,000 kutokana na uharibifu huo uliofanywa na Chris Brown.
Wiki iliyopita Chris Brown alishtakiwa na aliyekuwa meneja wake, Mike G kwa madai ya kumpiga ngumi usoni na shingoni bila hata kumfanya kitu

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top