Msanii wa mziki wa Dance Hall hapa Bongo, Chibwa amesema
kuwa tayari ameshafanya collabo kubwa tatu na wasanii wa nje ambazo
hazijatoka.
Tayari Chibwa ameshaachia collabo yake moja ‘Dancehall Digital’ ambayo amemshirikisha msanii kutoka Jamaica, Elephant Man.
Akiongea na Bongo5, Chibwa amesema, “Mpaka sasa nimeshafanya collabo tatu.”
“Wapo wasanii wengi kutoka nje nimeshafanya nao collabo lakini siwezi kuwataja kwa sasa kutokana na hili la video na Elephant Man bado kukamilisha kwa mashabiki zangu vizuri. Baadhi ya hizo collabo zitatoka mwaka huu,”ameongeza
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )