Bomoabomoa
ilianza mwishoni mwa mwaka 2015 kwenye baadhi ya maeneo Dar es salaam
hasa ya mabondeni na maeneo ya kando na mto Msimbazi ambapo zoezi hilo
lilisitishwa baada ya kesi kufunguliwa kupinga ubomoaji wa nyumba 2619 za wakazi wa Tabata Segerea mwigizaji Wastara akiwa miongoni mwao.
Wastara amekaa kwenye Exclusive Interview na millardayo.com na AyoTV leo na kusema yafuatayo >>> ‘Baada
ya kuona kuna bomoabomoa inakuja nikahangaika nikapata pesa ya kununua
nyumba sehemu nyingine ili nipate pa kuwahifadhi watoto wangu na watoto
yatima ninaowalea na kuishi nao’
‘Nimehangaika
kwa nguvu zangu kwa hela halali bila kupewa na mtu nikapata hiyo nyumba
nyingine, nashukuru pia baada ya kufikiria kupata nyumba mpya huku
kwenye nyumba zilizopigwa X tukapewa ruhusa ya kuendelea kukaa na
kutafuta leseni za makazi‘ – Wastara
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )