Featured
Loading...

Mtoto Aliyewekewa Betri Kwenye Moyo Kuruhusiwa Kupita Kwenye Viwanja vya Ndege Bila Kukaguliwa na Mashine


Kadi ya kumtambulisha mtoto Happiness John (5) kimataifa baada ya kufanyiwa upasuaji na kuwekewa betri ndani ya moyo inatengenezwa nchini Afrika Kusini. Happiness ambaye alifanyiwa upasuaji huo Julai 15 na kuruhusiwa kutoka hospitalini wiki moja iliyopita, anatakiwa kuwa na kadi tambulishi ambayo itamuwezesha kutofanyiwa ukaguzi wa kielektroniki. Kwa sasa mtoto huyo amepewa kadi ya muda ambayo inamruhusu kutopita katika maeneo yenye mionzi kwa ajili ya ukaguzi, ikiwamo viwanja vya ndege na majengo yenye ulinzi mkali.

Tuendelee kumtakia heri mtoto huyu

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top