January Makamba Mbunge wa jimbo la Bumbuli mkoani Tanga
…………………………………………………………………………………………………
Raisa Said, Bumbuli
Jumla ya vijiji 49 vya
Halmashauri ya Wilaya vitapata umeme katika awamu ya tatu ya Mradi ya
Umeme Vijijini ambayo imeanza hivi karibuni.
Akizungumza wakati wa
ziara ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo katika
halmashauri hiyo jana, Mbunge wa Jimbo la Bumbuli, January Makamba
aliishukuru serikali kwa kupeleka umeme katika hivyo na kusema kuwa
hatua hiyo inafanya vijiji vyote 90 vya halmashauri hiyo kufikiwa na
umeme baada ya awamu hiyo.
Makamba,ambaye pia ni
Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Mazingira
na Masuala ya Muungano alisema kuwa vijiji 50 vilipata umeme kupitia
mradi wa umeme vijijini katika awamu ya kwanza na ya pili.
“Tunakushukuru Waziri na serikali kwa ujumla kwa kuwapatia umeme wananchi wa Halmashauri ya Bumbuli,” alisema.
Naye Waziri wa Nishati
na Madini, Professor Sospeter Muhongo amesisitiza juu ya umuhimu wa
kupanga na kutekeleza mpango wa umeme vijijini kwa kuangalia kupanuka
kwa matumizi katika kipindi cha muda mrefu.
Professor Muhongo ambaye
yuko katika ziara mkoani Tanga kuangalia maendeleo ya shughuli za mradi
wa umeme vijijini, aliyasema hayo katika kijiji cha Mbuzii, katika
Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli, wilayani Lushoto mara baada ya kukagua
mashine ya kupozea umeme ya KVA 50 kijijini hapo.
Alikuwa anataka kujua kama mashine hiyo itatosheleza kuwadumia wananchi wa eneo hilo kama idadi ya watumiaji ikiongezeka.
Waziri huyo aliambiwa na
mashine hiyo itatosha kwa wakazi wapatao 1000 waliopo hapo kwa muda huu
na baada ya miaka miwili mitatu itabidi iwewekubwa zaidi ili kuhudumia
watu wengi zaidi.
“Tusifanye kazi ya mara mbili mbili. Tunapoweka miundo mbinu hii lazima tulenge matumizi ya miaka mingi hadi miaka 50,” alisema.
Alisema kuweka
miundombinu isiyoangalia matumizi ya uda mrefu siyo busara kwani hakuna
hakika kuwa hiyo miaka miwili au mitatu watumiaji wakiongezeka kutakuwa
na fedha za kununulia na kuweka mashine hizo. Alitaka utekelezaji wa
Umeme Vijijini awamu ya tatu ambayo ytayari imekwisha anza kuzingatia
suala la kuweka miundombinu ambayo itatumiwa kwa muda mrefu bila
kubadilisha.
Professor Muhongo
aliwataka wananchi wa vijijini kujiandaa kubadilisha uchumi wana maisha
yao kutokana na azma ya serikali kupelekea umeme mwingi vijijini.
“Tunaleta umeme mwingi
vijijini kwa sababu tunataka mabadiliko ya uchumi na ndiyo maana
serikali imeweka bajeti ya Sh. Trilioni moja kwa mwaka kupeleka umeme
vijijini na kuongeza idadi ya watumiaji wa umeme Tanzania kutoka
asilimia 40 ya hivi sasa hadi asilimia 75,” aliwaeleza wakazi wa
Bumbuli.
Profesa Muhongo alisema kuwa Tanzania haiwezi kujivunia mamendeleo wakati kuna watu bado wanatumia kibatali kwa ajili ya taa.
Hata hivyo, Waziri huyo
aliwataka watanzania kuwa wavumilivu na subira kwa sababu vijiji vyote
15,000 nchini haviwezi kupata umeme wakati mmoja. “Hata kule kwenye
jimbo langu, au hata anakotoka Rais, au Waziri Mkuu kuna vijiji ambavyo
havitajapata umeme. Tuwe wavumilvu ndugu zangu kwa sababu serikali
imeazimia kuleta umeme kwa watanzania wote,’ alisema.
Alieleza kuwa wakati wa
Bumbuli na maeneo mengine vijijini kujiandaa kuchakatua bidhaa zaona
badala ya kuuza bidhaa ghafi. “jiandaeni kuuza unga badala ya mahindi au
kuuza matunda yaliyokwisha kuchakatuliwa na kufungwa kitaalamu moja kwa
moja kwenye maduka ya vyakula makubwa badala ya mahindi au matunda
ghafi,’ alisema.
Akijibu swali moja
aliloulizwa na mwananchi mmoja juu ya taratibu za kupata umeme kwenye
makazi, aliiagiza Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kutembelea maeneo
yote ambayo yameletewa umeme au yana matarajio ya kupelekewa umeme ili
kuwaelezana kuwaelekeza wananchi juu ya taratibu za kujiunganisha na
umeme.
Shirika hilo litakuwa na
ziara august 25, mwaka huu katika vijiji vya Bumbuli kujibu na
kuelekeza kuhusu masuala mbalimbali ya taratibu za umeme.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )