Zaidi ya watu mia mashuhuri
walifika katika kusherehekea ya miaka 100 ya nywele za Kiafrika,
shughuli hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam tarehe 15 Agosti na
Ulikuwa ni uzinduzi wa kipekee.
Yote ilikuwa ni kuhusu uwezeshaji
wa mwanamke wa Kiafrika. kauli mbiu ya shughuli hii ilikuwa ni “Kila
ndoto ni halali” Usiridhie
Darling Group, kama kiongozi wa
soko la nywele na biashara za huduma ya nywele Afrika , walitambulisha
bidhaa zao mbalimbali za Aliyana professional kwa watengeneza nywele
wote nchini Tanzania. Tukio hilo pia lilipambwa na wanamitindo mahili wa
Tanzania
Wakati maonesho ya mavazi
yakiendelea, wageni walitambuliswa mfululizo wa bidhaa za nywele za
Aliyana Professional Shine na Aliyana Professional enrich zenye ubora
wa hali ya juu katika kuimarisha nywele.
Wanamtindo walipewa nafasi ya kubadilishana uzoefu na watengeneza nywele hodari ambao Tanzania inaweza kujivuna nao.
Tukio hilo lilibarikiwa na uwepo
wa mwakilishi wa Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo Mhe. Nape Nnauye.
Ambaye ni Mkurungenzi Idara Ya Sanaa na Utamaduni, Leah Kihimbi.
Mwakilishi mwandamizi wa kampuni
hiyo hapa Tanzania, alizungumza kuhusu kundi hilo changa la Godrej Group
lenye miaka 119 likiwa na uongezeko la uwepo wake barani Afrika,
Amerika ya Kusini, na Asia.
Kundi hilo la Godrej Group ni
wamiliki wa Darling Group katika nchi 14 za Afrika, ambapo Darling ni
kiongozi wa soko la nywele na huduma za nywele.
Msemaji wa kampuni hiyo
aliwakaribisha wageni waalikwa na kuwaambia kuwa sehemu ya safari hii
ya kusisimua nchini Tanzania, sababu bidhaa mbalimbali za Aliyana
Professional ni kutokana na uimara wake.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )