Afisa
Tarafa wa Ukonga Bw. Jeremiah Makorere akifafanua jambo kwa Waziri wa
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi wakati wa ziara
ya waziri huyo kubaini migogoro mbalimbali ya ardhi katika eneo la Pugu
Jijini Dar es Salaam.

Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akizungumza
na wananchi wa Mtaa wa Guluka Kwalala kata ya Gongo la Mboto jijini Dar
es Salaam ambao wamevamia eneo la Kilichokuwa kiwanda cha nguo cha
KiliTex.

Mmoja ya
Fundi gereji katika Mtaa wa Guluka Kwalala kata ya Gongo la Mboto jijini
Dar es Salaam Bw. Mohamed Ali akielezea sababu za wao kuvamia eneo la
Kilichokuwa kiwanda cha nguo cha KiliTex kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi (hayupo pichani).

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimsikiliza kwa makini Afisa Ardhi toka Manispaa ya Ilala Bw. Furaha Mwakapalila akielezea historia ya eneo la Kilichokuwa kiwanda cha nguo cha KiliTex ambalo kwa sasa limevamiwa na mafundi magari wa kata ya Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )