Featured
Loading...

Majibu ya Gavana wa Benki Kuu, Prof Ndulu kwa wanaosema pesa imepotea


Leo September 14 2016 Gavana wa benki wa Benki kuu ya Tanzania Prof. Benno Ndulu ameitoa taarifa kuhusu hali ya uchumi ambapo amesema uchumi wa nchi kwa robo ya kwanza ya mwaka 2016 ukuaji wa Pato la Taifa unakadiriwa kuongezeka kwa asilimia 5.5 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 5.7 kipindi kama hicho mwaka 2015.
Prof. Ndulu ametaja vitu vilizochangia ukuaji huo wa uchumi kwa kiasi kikubwa ni pamoja na kilimo (asilimia 11.7) biashara (asilimia 10.6), uchukuzi (asilimia 10.1), sekta ya fedha (asilimia 10.1) na mawasiliano (asilimia 10.0). Shughuli za kiuchumi zilizokua kwa kasi ya juu zaidi katika robo ya kwanza ya mwaka 2016 ni sekta ya fedha (asilimia 13.5), mawasiliano (asilimia 13.4).
Akijibu baadhi ya malalamiko kuwa fedha kwa sasa imepotea Prof. Ndulu amesema ………>>>’hii hisia ya kusema fedha imepotea, mimi nadhani kwenye hili ni muhimu tukaelewa hisia zinakuja kwa sababu gani, serikali imechukua hatua kubwa za kuongeza mapato kwa hiyo imeimarisha ukusanyaji kodi imeziba mianya ya ukwepaji kodi’
Aidha Serikali katika matumizi yake imebana shughuli za wale waliokuwa mission town na shughuli hizi zilizo nyingi zinafanyika kwa uwazi

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top