Mbunge
wa Arusha Mjini Godbless Lema amesema hata kama gharama za matibabu ya
Tundu Lissu yakifika Trilioni moja, watakuwa tayari kuuza figo zao.
Akizungumza
jana Novemba 18 katika kata ya Siuyu iliyopo Wilaya ya Ikungi mkoani
Singida Lema alisema utekelezaji wa majukumu ya kisiasa ukiwa upinzani
wakati huu ni ngumu kutokana na kuwindwa kila uchao.
Alisema
pamoja na ugumu huo hawajarudi nyuma na kisasi cha wasiopenda
mabadiliko na wanaochukia kukosolewa kimedhihirika kwa vitendo
alivyotendewa Lissu.
"Lissu
yupo kitandani risasi mwili mzima, gharama za matibabu yake ni kubwa,
lakini hata ikifika trilioni moja na tukawa hatuna fedha tutauza figo
zetu kuendelea kugharamia matibabu yake" alisema Lema.
Alisema Lissu amekuwa alama ya haki katika taifa kutokana na kuamua kuwa upande wa haki.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )