Umoja
wa Vijana UVCCM, umeunda kamati ya kufuatilia vitega uchumi na mali za
umoja huo nchi nzima. Kamati hiyo inaundwa na wajumbe nane na itaongozwa
na Mariam Chaurembo.
Kaimu
Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka amesema kamati hiyo inakwenda
kuchunguza na kuangalia vitega uchumi na mali zote za umoja huo.
"Mwenyekiti ameanza na kazi hii ili aweze kujua mali na vitega uchumi na umoja viko katika hali gani na vinaendeshwaje,"
"Wajumbe
hawa watafanya kazi hiyo kuanzia leo wakiangalia na kufuatilia,
kuchunguza, kuorodhesha mali za chama na mapato yanayotokana na vitega
uchumi hivyo zinakwenda wapi," amesema Shaka
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )