Ofisa
Mfawidhi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu
(Sumatra) mkoa wa Kigoma, Amaniel Sekulu amesema miili sita ya watu
waliozama katika ajali ya boti kugonga mtumbwi katika Ziwa Tanganyika
imeopolewa.
Mpaka
sasa idadi ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo iliyotokea
Ijumaa iliyopita imefikia 19 kutokana na awali kuopolewa miili 13.
Akizungumza leo Jumapili Desemba 24, Sekulu amesema miili hiyo sita imeharibika kutokana na kukaa majini zaidi ya saa 50.
Amesema
uopoaji wa miili hiyo ilikumbwa na changamoto kadhaa, ikiwemo wazamiaji
kukumbana na hali mbaya ya hewa, mvua za mara kwa mara, mawimbi makubwa
na kina kirefu cha maji.
Amesema
Jeshi la Polisi, Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na wananchi wenye
ujuzi wa kuogelea ndio waliofanikisha kupatikana kwa miili hiyo.
Ajali
hiyo ilitokea usiku wa kuamkia Ijumaa ikihusisha boti la Atakalo mola
lililokuwa linatoka Kigoma mjini kwenda Kalya na mtumbwi wa MV Pasaka
uliookuwa ukitoka kijiji cha Kalilani kwenda Sunuka.
MV
Pasaka ilikuwa imebeba waumini wa Kanisa la Pentekoste waliokuwa
wanakwenda kwenye mkutano wa injili na sherehe za sikukuu Krisimasi
katika kijiji cha Sunuka.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )