Jeshi
la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linawashikilia watu wawili kwa
tuhuma za kutumia sare za Jeshi la Wananchi nchini (JWTZ) kufanya
matukio mbali mbali ya kihalifu.
Wakati
akizungumza na wanahabari jana Disemba 22, 2017 jijini Dar es Salaam,
Kamanda wa Kanda hiyo, SACP Lazaro Mambosasa, aliwataja watuhumiwa hao
kuwa ni Lainon Fratenus (20) na Noel Cleophace Wagesa (30) wote wakazi
wa Kigogo.
“Jeshi
la Polisi mnamo Disemba 15, 2017 majira ya saa sita usiku maeneo ya
Lugalo Kawe polisi wakiwa dolia walifanikiwa kukamata wahalifu wawili
wakiwa wamevalia sare za JWTZ na kisu kimoja huku wakitumia gari namba T
306 CRU Toyota Carina rangi ya fedha, wanatuhumiwa wanasadikiwa
kujihusisha na matukio mbalimbali ya uporaji jijini Dar es Salaam,”
amesema.
SACP
Mambosasa amesema watuhumiwa wanaendelea kuhojiwa ili kubaini mtandao
mzima na matukio yote waliyowahi kufanya na baada ya upelelezi
kukamilika watuhumiwa watapelekwa mahakamani kwa hatua zaidi za
kisheria.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )