Jeshi 
 la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wanatarajia kuwa wenyeji wa 
zoezi la mafunzo yaitwayo Ushirikiano imara 2018 litakaloshirikisha nchi
 za Afrika Mashariki zikiwemo Burundi, Rwanda, Kenya na Uganda ambapo 
mafunzo yataendeshwa mkoani Tanga .
Akizungumza
 na wanahabari jijini Dar es salaam Mkuu wa Mafunzo na Operesheni  
(JWTZ) Meja Jenerali Alfred Fabian Kapinga amesema kuwa, zoezi hilo ni 
la medani na litafanyika katika wilaya za mijini pamoja na Wilaya ya 
Muheza mkoani Tanga.
Ameeleza
 kuwa zoezi hilo litaanza rasmi tarehe 05 mpaka 21, sambamba na hilo 
mafunzo hayo yatalenga kujenga uwezo wa kukabiliana na uharifu pamoja na
 majanga.
Pia
 amesema kuwa dhumuni la zoezi hilo kikanda ni kubadilishana uzoefu wa 
kiutendaji, kuimarisha mahusiano baina ya nchi, majeshi ya Afrika 
Mashariki pamoja na taasisi zingine za kiraia ambazo zitashiriki zoezi 
hilo.
Sanjari
 na hilo kutakuwa na kazi za kusaidia jamii katika shughuli mbalimbali 
zikiwemo ujenzi wa madarasa, ofisi za walimu pamoja na vyoo katika Shule
 ya msingi ya Machemba iliyopo Wilaya ya Muheza mkoani Tanga, pia 
kutakuwa na utoaji wa huduma za tiba kwa wananchi katika eneo la zoezi.
Hivyo,
 Meja Fabian ametoa rai kwa wakazi wa Tanga kuonyesha ukarimu pamoja na 
amani baina ya wageni watakaokua kwa kipindi chote cha mafunzo kama 
walivoonyesha mwaka jana ambapo mafunzo yalikua yakiendeshwa.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
 

 
 
 
 
 
 
 
