Featured
Loading...

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 35 & 36 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )


Mtunzi:EDDAZARIA G.MSULWA

Ilipoishia...

Daktari aliye kuwa anaendelea kunipiga baada ya kumuona mwenzake akiwa anaaga dunia akaniacha na kwa nguvu zake zote akarusha kirungu chake na kikatua kichwani mwa sheila na akadondoka chini na damu za puani zikaanza kumwagika

Endelea....
Taratiu nikaanza kujiburuza chini hadi sehemu aliyo angukia sheila huku machozi yakinimwagika na kujikuta nikijilaza juu yake na kumfanya daktari aliye mpiga akanza kunipiga tena kwenye mgongo akinimrisha nimuechie sheila ili aendelea kumshuhulikia kwa kipigo.Kila nilipo jaribu kumtingisha sheila sikuweza kuona dalili yoyote ya kuishi kwake na kujikuta nikizidi kumkumbatia kwa uchungu.Nikaanza kusikia makelele yakija kwa nyuma yangu,nikageuza shingo yangu na kuona kundi kubwa la vichaa wakija kwa kasi na kumfanya daktari anaye nipiga kutimka mbio na sikujua ni wapi anapo elekea na wote wakanipita na kuendeleka kumkimbiza dakrari aliye kuwa akinipiga.

Nikaona nikiendelea kujiliza haita saidi zaidi ya kumfanya sheila kuzidi kuzidiwa na kipigo alicho kipata.Nikajikaza na kwabahati nzuri miguu yangu ina nguvu za kutosha nikanyanyuka na kujinyoosha japo nilijawa na maumivu makali ila sikuwa na jinsi.

Nikanyanyua sheila na kutokana na kudhohofika kwake kwa mwili haikuwa ngumu kwangu kumbeba hadi tukafika kwenye kwenye moja ya ofifisi na kuwakuta vichaa wakiwashambulia manesi waliomo ndani ya ofisi.Hali ya hospitali imechafuka kupita maelezo madaktari wanashambuliwa na vichaa ambao wamepandwa na hasira.Kwa bahati nzuri nikaona gari moja ya waogonjwa amayo imesimama nje kwenye maegesho huku dereva wake akichomolewa kwenye gari na kuanza kupewa kipigo kama ilivyo kwa wahudumu wengine wa hospitali ikiwemo walinzi.

Hapa ndipo nikagundua kuwa vichaa tunafahamiana kwa maana kwa kila nilipo pita huku nikiwa nimembeba sheila hapakuwa na anaye nigusa tofauti na wanapo muona muudumu wa hospitali hii.Nikafanikiwa kufika kwenye gari la wagonjwa nakumuingiza ndani ya gari sheila na kwenda upande wa dereva na kuanza kutafuta fungua na sikuweza kuiona ikanibidi nishuke na kuunza kuupapasa mwili wa dereva ulio lala pembezoni mwa gari na kwabahati nzuri nikaiona funguo kwenye mfuko wake wa suruali.

Nikawasha gari na kuondoka hukiwasaidia vichaa kutoka ndani ya hospitali hii baada ya kuligonga geti lililokuwa kimefungwa.Kutokana sikuwa ni mwenyeji sikujua ni wapi nielekee ili kumuwahisha sheila hospitali.Nikasimamisha gari pembezoni mwa arabara huku likiwa linawaka ving’ora na kuichukua simu iliyopo ndani ya hospitali na kuanza kubuni namba ya baba

Kwa mara ya kwanza ikapokelewa na mwanamke ambaye hata lugha hatulewaa na nikajua nitakuwa nimekosea,nikajaribu kufikiria namba nyingi ambazo zinaweza kufanana na namba ya baba na pia namba niliyo ipiga ikapokelewa na kijana na akaanza kumwaga matusi alipoona sizungumzi kitu chochote baada ya kusema haloo.Nikajaribu zaidi ya mara saba nipo kumbukumbu ya namba za baba ziliponijia vizuri kichwani na nikaipiga ikaita kwa muda kisha ikapokelewa
“nani mwenzangu?”
Ilikuwa ni sauti ya baba na kidogo tabasamu likanijia usoni
“mimi eddy”
“eddy……!!”

“ndio ni mimi baba ninaomba msaada wako”
Upo wapi mbona makelele ya king’ora?”
“nipo kwenye gari ya wagonjwa nimetoroka hospitalini ila mimi sio kichaa kama ulivyo dhania”
“ngoja kwanza umesema upo wapi?”
“mimi hapa wala sipajui ila kuna magorofa mafupi mafupi hii na kuna magari mengi yamesimama pembeni”
“umesema upo kwenye gari ya wagonjwa?”

“ndio”
“wewe ndio dereva ua kuna dereva?”
“mimi ndio dereva”
“sasa angalia kwenye upande wa kusoto kuna kijitivii kidogo….”
“ndio nimekiona”
“kiwashe kama hakija washwa na kwenye sehemu ya chini yake kuna batani nane umeziona”
“ndio”

“minya batani iliyo andikwa map”
Nikaiiminya batani ambayo baba aliniambia na ndani ya sekunde kadhaa kukatokea ramani yenye mistari mingi mingi huku kukiwa na kialama chekundu kikiwa kina waka waka
“inakisoma vipi hiyo ramani?”
“inasoema cape town, western cape city”
“subiri tunakuja sasa hivi”

Nikakata simu na kuzima gari na kufungua kijidirisha kilichopo nyuma ya siti yanga na kumuona sheila akiwa amejilaza huku akipumua kwa shida kidogo nikapata matumaini.Ndani ya nusu saa gari mbili zikasimama mbele ya gari nililipo na mtu wa kwanza kushuka ni baba na moja kwa moja akafika kwenye gani na akaonekana kunishangaa jinsi damu zinavyo nivuja.Watu wake wakanitoa ndani ya gari
“baba kuna mtu mwengine huku nyuma”
“ni nani?”
“rafiki yangu”

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top