Featured
Loading...

Rasmi:40 ya Mdogo Wake Tiffah Yaota Mbawa,Chanzo cha Yote Hayo Ni hiki Hapa..!!!

 
dimond-1
Desemba 6, mwaka jana Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ alipata mtoto wa pili kupitia kwa mzazi mwenzake, Zarina Hassan ‘Zari’ na kumpa jina la Nillan Nasibu ‘Chibu Junior’, akiwa ametanguliwa na dada yake, Latifah ‘Tiffah’ aliyezaliwa Agosti 6, 2015.

 
Kwa hesabu za harakaharaka, Januari 16, mwaka huu, Nillan alikuwa anatimiza siku 40 tangu kuzaliwa kwake, lakini siku hiyo imepita kavukavu huku wadau wake waliokaa mkao wa sherehe wakibaki na maswali bila majibu.
SHUGHULI ILIKUWA KWENYE RATIBA
Wiki chache zilizopita, iliripotiwa kwamba, Diamond kwa maana ya baba wa mtoto, aliandaa sherehe ya kufa mtu ambayo ingefanyika jijini Johannesburg, Afrika Kusini ‘Sauzi’ ambako mtoto huyo alizaliwa.
“Lakini kinachotushangaza wadau ni kwamba, mpaka siku zinakaribia hakuna dalili na matokeo yake, siku imepita hakuna lolote.
“Tulipewa kadi watu ambao tungekwenda Afrika Kusini kwenye shughuli. Lakini naona kimya kingi mpaka Januari 16 imepita. Hakuna cha 40. Hata kama shughuli itafanyika Jumamosi hii (keshokutwa) itakuwa si 40 tena, bali ni 45 sasa,” kilisema chanzo hicho.
TOFAUTI NA TIFFAH
Baadhi ya wadau wa staa huyo sambamba na mashoga zake Zari waliliambia Amani kuwa, ujio wa Nillan hauna ‘vurugu’ kama ilivyokuwa kuzaliwa kwa Tiffah ambaye nchi ilisimama.diamond-tiffahs-40-2
Siku ya 40 ya Tiffa
“Unajua huenda 4O ikawa imepoteza mvuto baada ya ile ya Tiffah kuchukua nyota yote. Utakuwa unakumbuka mwandishi kwamba, kuzaliwa kwa Tiffah Bongo ilitulia kimya. Hata siku ya 40 yake kule nyumbani na baadaye kwenye ile shughuli ya Mlimani City, jina la Tiffah lilikuwa juu sana.”diamond-tiffahs-40-3
Siku ya 40 ya Tiffa
WENGI HAWAMJUI NILLAN
“Lakini sasa  we fanya utafiti wa kawaida tu, Wabongo wengi hawalijui jina la Nillan ambaye ni mdogo wake Tiffah. Hakuna mbwembwe wala matangazo,” kilisema chanzo.diamond-7
Prince Nillan Dangote
MABENKI YAMECHANGIA?
Habari zaidi zinasema kuwa, mbwembwe za Tiffah mwaka juzi zilichangiwa na mabenki yaliyojitoa kumwaga pesa kwa ajili ya kuchukua haki ya kwanza ya kumwonesha sura mtoto  huyo ambapo tofauti na ujio wa Nillan, hali ya mabenki imekuwa mbaya kiasi kwamba, yale mawili yaliyotaka kuchukua haki hiyo yaliingia mitini.
“Ukifuatilia kwa karibu hapo utabaini kuwa, kutojitokeza kwa mabenki hayo kumwaga pesa pia kumechangia kudorora kwa vuguvugu la kuzaliwa kwa mtoto Nillan.
“Unajua hali ya uchumi ni mbaya kwa sasa, nadhani hata Diamond mwenyewe anajiuliza kama akifanya sherehe kubwa ya 40 halafu akatumia mfano milioni hamsini kama staa yeye atafaidika na nini? Sherehe  tu? Maana kama ni mtoto anaye tena ni wa pili huyu.”
MAMA DIAMOND AREJEA BONGO, AJICHIMBIA MADALE
Awali ilidaiwa kuwa, baada ya mama Diamond, Sanura Kasim ‘Sandra’ kwenda Sauzi kusubiria Zari kujifungua Nillan, ratiba ilimtaka aendelee kutulia kulekule akisubiri 40 ambayo ingefanyika kule lakini habari zinadai kutokana na kutokuwepo kwa ishu hiyo, mwanamke huyo amerejea kimyakimya Bongo na amejichimbia Madale nyumbani kwa mwanaye.mama-diamond
Diamond, mama Daimond kulia Rommie Jons
“Kama mnataka kujua kuwa 40 imebuma, hata mama Diamond amerudi. Hivi ninavyoongea na wewe mwandishi, mama amejaa tele Madale. Hakuna mbwembwe. Ama kweli hali ya uchumi wa mifuko ni mbaya jamani,” kilisema chanzo.
ZARI NAYE ATUA BONGO
Habari zaidi za chini kwa chini zinasema kuwa, mama Nillan, yaani Zari naye ametua Bongo bila mbwembwe hali inayotoa taswira ya kutokuwepo kwa shughuli achilia mbali sherehe.
BABA DIAMOND AFUNGUA BEGI
Ikazidi kudaiwa kuwa, baada ya kuvunjika kwa safari ya Sauzi, baba wa Diamond, mzee Abdul ambaye aliwahi kuripotiwa kuwa, amekaa mkao wa safari, ilibidi afungue begi na kutoa viwalo vyake kisha kuendelea na maisha yake ya kila siku, Bongo.
MADAI YACHUNGUZWA
Ilibidi Amani lishike nyuzi hewani ili kuwasaka wahusika hao. Mtu mgumu sana kupatikana katika wote ni Zari ambaye uchunguzi unaonesha kuwa, hata wale madansa wa Diamond, akina Moses Iyobo hawana namba yake au wamepigwa marufuku kwa kiapo kuigawa.
Hivyo Amani lilimtafuta Diamond mwenyewe kwa njia ya simu yake ya mkononi iliyoita weee mpaka ikakatika bila kupokelewa.
Amani likaona isiwe shida, likamtumia meseji (SMS) kwa kuamini kwamba, kama alipopigiwa alikuwa anaoga, anaendesha gari, anapafomu au yuko faragha, baada..
ya kuiona meseji hiyo angejibu lakini wapi!
MAMA DIAMOND
Ndipo Amani likamgeukia mama Diamond mwenyewe ambaye ndiye anayetajwa kusimamia maandalizi ya shughuli au kuamua kutosimamia kuandaa ambapo hali ilikuwa hivi:
Amani: (latoa utambulisho wa jina na chombo cha habari).
Mama Diamond: Aha! Niambie, unataka kunifundisha uandishi wa habari?
Amani: Ndiyo.
Mama Diamond: Haya nipe habari, nakusikiliza.
Amani: Napenda kujua, kuna madai kwamba, shughuli ya 40 ya mdogo wake, Tiffah imeota mbawa, hakuna. Je ni kweli au imeshafanyika kimyakimya?
Mama Diamond: (akakata simu).
Amani liliamini kuwa, huenda simu hiyo imekatika kutokana na hali ya mtandao, likaacha zikatika dakika kumi kwanza kabla ya kupiga tena.
Baada ya dakika kumi kupita…
Mama Diamond: We nani?
Amani: Mimi ni …(utambulisho wa jina na chombo cha habari).
Mama Diamond: (akakata simu).
BABA DIAMOND
Kwa upande wake, baba Diamond alipotafutwa na kuulizwa kuhusu safari hiyo alisema yeye ni msikilizaji kama safari ipo angekwenda kama haipo pia hana neno.
“Mimi ndugu yangu ni wa kusikiliza tu. Kama safari ipo nakwenda, kama haipo hakuna neno. Kikubwa ni kumwomba Mungu atupe uzima,” alisema.

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top