Kiongozi wa upinzani Kenya Raila Odinga
leo amerejea nchini humo akitokea Marekani na kupokelewa na maelfu ya
Wananchi kuanzia uwanja wa ndege.
Inaripotiwa kwamba fujo zimetokea baada
ya Polisi kuingilia kati msafara huo ambapo zimesababisha vifo vya watu
wawili huku Basi moja la Abiria (Matatu) likiteketezwa kwa moto pamoja
na Lori moja la Polisi.
Mahakama ya juu nchini Kenya inatarajiwa
kutoa uamuzi wake kuhusu uhalali wa Uchaguzi wa Tarehe 26 October
ambapo Uhuru Kenyatta aliibuka mshindi huku Raila Odinga akiususia
uchaguzi huo kwa kutoshiriki.
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )