Featured
Loading...

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 7 & 8

Muandishi : Eddazaria g.Msulwa


Ilipoishia
Askari mmoja mwenye mwili mkubwa akamnyanyua Fetty na kumuweka begani mwake na safari ikaendelea.Fetty akayafumbua macho yake na kuona askari aliye mbebe ndio wa mwisho katika mstari wanao tembea,Kwa ustani wa hali ya juu Fetty akaichomeka mikono yeke katikati ya shingo ya askati,kwakutumia pigu akaanza kumnyonga askari huku akiwa amening'inia kwa nyuma.Mikoromo ya asakri ikawastua wenzake waliopo mbele kitendo cha wao kugeuka wakamkuta mwenzo ndio yupo kwenye hatua za mwisho huku macho yake akiwa ameyatoa njee

ENDELEA
Askari mmoja akataka kufyatua risasi ila mkuu wa masafara akamzuia,Fetty akaiachia shingo ya askari huku akiwa amehakikisha kwamba askari huyo yupo kwenye hali mbaya sana.Askari mmoja akampiga Fetty kwa kutumia kitako cha bunduki na kumfanya  Fetty ajikunje huku akitoa mguno mkali wa maumivu
“Kumbukeni kuwa,anahitajika akiwa hai”
Mkuu wao alizungumza

“Sawa mkuu,ila anahitaji kupata kibano kidogo”
Wakaendelea kumtazama mwenzo,ambaye hadi hapa alipo hali yake haipo vizuri sana.Vichwa vya askar vikaanza kupata moto kwani mwenzao ambaye alikuwa anakaribia kunyongwa ndio anaye fahamu njia ya bombo hilo japo imenyooka ila kuna sehemu mbele imegawanyika katika njia nne.Mwenzao anayejulikana kama inspector Julio hawezi kuendelea mbele na safari

“Mkuu kuna tatizo jengine limejitokea,Over”
“Nini tena inspector John? Over”
“Huyu binti alimkaba Inspector Julio,Over”
“Nyinyi mulikuwa wa hadi mwenzetu akabwe?”
Sauti ya mkuu wao ilizungumza huku akiwa anafoka,
“Mkuu alizimia,ndipo inspector Julio alipo amua kumbeba”
“Pumbavu zenu.Hakikisheni anatoka huyo binti,akiwa hai na Julio naye akiwa hai”

Fetty akatabasamu huku akiwatazama askari,kwani kwake kazi yake imeshaanza kuwa nyepesi kwani mtu ambaye anamuhofia ni huyu Inspector Julio,ambaye kwa mtazamo wake tu anaonekana ni mtu hatari sana katika swala zima la kutumia silaha.Askari mmoja akasimama mbele ya Fetty huku akiwa amempa mgongo akisaidiana na wezake katika kumpa huduma Inspector Julio,huku kazi yake ikiwa ni kuzifungua kamba za viatu vya Julio

Kwa umakini wa hali ya juu,Fetty akazichomoa funguo nyingi zinazo ning’inia kiunoni mwa askari huyo pasipo yeye mwenyewe kujua.Kwa bahati nzuri katika wingi wa funguo hizo zipatazo kumi na mbili,mbili ni funguo za pingu.

Macho ya Fetty yakawa na kazi ya kuwatazama askari jinsi wanavyo pata shida katika kumsaidi mwenzao ambaye hali yake inazidi kuwa mbaya.

Hakuna askari aliye kuwa na muda wa kumtazama Fetty kwani wanaamini kile kitako cha bunduki alicho pigwa kwenye tumbo,bado anaendelea kukisikilizia maumivu yake.Fetty akafanikiwa kufungua pingu za mikono pasipo askari yoyote kugundua.Akajaribisha kufungu mnyororo wa miguni ila akashindwa kwani hakuna funguo inayo ingiliana na kufuli alilo fungwa miguuni.

“Ja............ama..ani mmmim...i siwezi ku...pona.Ila,njia uki...oony......sha utaku...nja kulia...kwenye shimo lenye mlang....o wa....”
Inspector Julio alizungumza kwa shida na hakuweza kumalizia sentesi yake,mauti yakamchukua.

Inspector John akanyanyuka kwa hasira na kumfwata Fetty sehemu aliyo kaa.Kufumba na kufumbua akajikuta akirushwa juu kimo cha mbuzi  tena beberu na kutua chini kama mzigo.

Hii ni baada ya Fetty kuikutanisha miguu yake kwa pamoja,Kisha mikono yake aliikita chini na kujizungusha kwa kasi kubwa.Askari walio salia wakiwa wanamtizama mkuu wao.Fetty akajinyanyua kwa haraka na kumvaa askari aliye mchomolea funguo,akaichomoa bastola ya askari huyo ambaye alijitahii kumpiga ngumi  za mbavu Fetty

Bila ya huruma Fetty akafyatua risasi iliyo penya kwenye kichwa cha akari anayepambana naye na kumtuliza kimya.Askari watatu wa kiume wakazikoki kwa haraka bunduki zao na kuanza kuzifyatua risasi,ila kwa haraka sana kama tairi la gari liendalo kwa kasi sana,akawa na kazi ya kubiringika huku akiwafwata askari kwenye miguu yao mita chache kutoka alipo.

Akiwa anabiringika, bastola iliyopo mkononi mwake ikawa na kazi ya kufyatua risasi zilizo waangusha askari watatu chini na akabaki Inspector John na askari wa kike aliyetengenezwa kama yeye,na wakati wote tukio  la wezake kuangamizwa lilimpa kiwewe hadi akawa na kazi ya kuyaziba masikio yake akiziba asisikie milio ya risasi.Fetty akalala katikati ya miguu ya Inspector John huku mdomo bastola yake akiwa ameuweka kwenye sehemu za siri za Inspector John.Bunduki ya inspector John akawa ameilekezea kwenye kichwa cha Fetty ambaye macho yake yanatazamana na macho ya Inspector  John
“Shoot ni kushooti”
Fetty alizungumza huku akitabasama,na bastola yake akawa na kazi ya kuigusisha gusisha kwenye vitenesi vya Inspector John

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
© Copyright MZALENDO HURU
Back To Top